HII HAPANAAAAAA:MAJAMBAZI WAVAMIA KANISA NA KUIBA

WATU wasiofahamika wamevunja Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa Jimbo la Iringa leo usiku, na kumjeruhi vibaya mlinzi wa Kanisa hilo Bw. Bathlomeo Nzigilwa.

Akitoa maelezo juu ya tukio hilo mhuduma wa Kanisa la jimbo kuu Kihesa, Sista Lucy  Mgata amesema aligundua uvamizi huo alfajiri baada ya kufika kanisani hapo kwa ajili ya ibada ya Misa za kila siku.

Majambazi hao wamevunja pia ofisi ya parokia na kuharibu vitabu na kumbukumbu mbalimbali zikiwa zimechanwa, huku Mavazi ya ibada na vifaa mbalimbali kama misalaba ikiwa imevunjwa.
 
Aidha Sista Mgata amesema watu hao wamechukua fedha  za watumishi walizokuwa wakichangishana, pamoja na hela za chama cha kitume cha utume wa Fatima japo bado hazijajulikana ni kiasi gani.

Hata hivyo Padre Aloyce Mdemu ambaye pia ni Makamu wa Askofu wa jimbo hilo, amesema bado ni mapema kujua thamani ya uharibifu uliofanyika, kwa kuwa wanaendelea na uchunguzi wa vifaa vingine na maeneo mengine ambayo huenda hawajayabaini.

Muuguzi mfawidhi wa hospitali ya Mkoa wa Iringa Bi. Rustica Tung’ombe amethibitisha kumpokea majeruhi Batromeo Nzigilwa, na kusema kuwa hali yake ni mbaya na  kuwa anaendelea kupata matibabu.
                                                                  
                                                               Source:Blogzamikoa

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post