WATOTO WAWILI WAFARIKI DUNIA PAPO HAPO NA MMOJA KUJERUHIWA BAADA KUANGUKIWA UKUTA CHAKAVU WA NYUMBA -SHINYANGA

Watoto wawili wamefariki dunia papo hapo na mmoja kujeruhiwa baada ya kuangukiwa na  ukuta chakavu wa nyumba  waliokuwa wanauchezea katika Kitongoji cha Galamba Kata ya Kolandoto Wilaya Shinyanga.

Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 12 jioni  katika kitongoji hicho.

 Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Evarist Mangalla amewataja watoto waliofariki dunia kuwa ni Neema Masanja(5) na Emmanuel Masanja (3) na mtoto aliyejeruhiwa kuwa  ni juma ngusa (3) ambaye amelazwa katika hospitali ya Kolandoto kwa ajili ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post