Semina ya siku 4 kuhusu uandaaji na usambazaji wa habari kupitia njia ya mtandao-ONLINE JOURNALISM yakamilika mjini Kahama

Mchambuzi wa mfumo wa computer Lukelo Mkami akifundisha namna ya kufungua blog na kutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kupashana  habari katika ulimwengu wa sasa wa sayansi na teknolojia mafunzo ya siku 4 yaliyokamilika jana ALHAMIS mjini Kahama mkoani Shinyanga

Miongoni mwa washiriki wa mafunzo hayo kushoto ni Suzy Butondo mwandishi wa gazeti la Mwanachi,kulia ni Wezay Ally kutoka Radio Faraja wakifungua Blog tayari kuanza kuandika habari kwenye mtandao wa intaneti.
Muda mchache baada ya mafunzo ya siku nne yaliyoandaliwa na UTPC kukamilika ,hapa ni ndani ya ofisi ya mkuu wa wilaya  ya Kahama Benson Mpesya,aliyesimama wa tatu kutoka kushoto ni meneja wa Radio Kahama Marco Mipawa,mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo akimkaribisha mchambuzi wa mifumo ya kompyuta Lukelo Mkami ili atambulishe rasmi aina mpya ya uandishi wa habari hapa nchini

Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya wakati wa zoezi la kutambulisha aina hiyo ya uandishi wa habari katika wilaya hiyo na mkoa wa shinyanga kwa ujumla uliofanywa na mchambuzi wa mifumo ya kompyuta kutoka muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania UTPC Lukelo Mkami,ambapo mkuu huyo wa wilaya aliwataka waandishi wa habari kuchangamkia fursa mbalimbali za mafunzo yanayotolewa na muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzanua  UTPC hali ambayo itawasaidia kuongeza ujuzi katika utendaji wa kazi zao na kuongeza kuwa serikali inatambua sana umuhimu wa waandishi wa habari hapa nchini.
Na mimi Mkurugenzi wa malunde1.blogspot.com ,Kadama Malunde ,Kushoto nikaamua kupiga picha na mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga ,Shija Felician,ambapo aliwataka waandishi wa habari kukubali mabadiliko ya kiteknolojia
Picha ya pamoja kwa baadhi ya  washiriki wa mafunzo hayo wa pili kutoka kushoto ni mchambuzi wa mfumo wa kompyuta kutoka muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania UTPC Lukelo Mkami,ambaye alikuwa mkufunzi wa mafunzo kuhusu  mfumo  mpya wa uandishi wa habari kwa njia ya mtandao wa intaneti yaliyodumu kwa siku 4 na kuwakutanisha waandishi  18 kutoka mkoa wa Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post