KIJANA AUAWA KWA KUPONDWA MAWE NA WANANCHI BAADA YA KUVAMIA NYUMBA YA MTU KWA PANGA NA KISU

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Evarist Mangalla





Kijana mmoja aitwaye Juma Masasila 25-30 ameuawa kwa kushambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi kwa kupigwa mawe  baada ya kuvamia nyumba ya mkazi mmoja katika kijiji cha Lunguya tarafa ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Evarist Mangalla kwa vyombo vya habari tukio hilo limetokea tarehe 13 Octoba mwaka huu  majira ya saa tano na nusu usiku ambapo Juma Masasila aliuawa kwa kushambuliwa na wananchi kwa kumpiga mawe na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababisha kifo chake papo hapo.

Chanzo cha mauaji hayo kuwa ni kitendo cha marehemu kuvamia nyumbani kwa bwana Amos Makoye kwa nia ya kumkata panga ndipo mkazi huyo alipopiga kelele kuomba msaada  hali iliyosababisha wananchi kufika eneo la tukio na kuanza kumshambulia marehemu.

 Kamanda Mangalla amesema  katika eneo la tukio kuliokotwa panga moja na kisu vitu ambavyo vinasadikiwa kuwa ni silaha alizokuja nazo marehemu kwa ajili ya kumcharanga bwana Amos Makoye na kuongeza kuwa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusika na tukio.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post