MAUAJI TENA-----! KIJANA AUAWA KIKATILI BAADA YA KUIBA KUKU- SHINYANGA

kijana mwingine ameuawa kwa kupigwa mawe na kisha mwili wake kuchomwa moto na wananchi baada ya kutuhumiwa kuiba kuku wanne katika kijiji cha Mawimilu kata ya Mwakitolyo tarafa ya Nindo wilaya ya Shinyanga vijijini.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Evarist Mangalla tukio hilo limetokea Octoba 17 mwaka huu jioni ambapo  kijana asiyefahamika jina wala makazi yake mwenye umri  wa miaka kati ya 25-30 aliuawa kwa kushambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi kwa kumpiga mawe na fimbo kisha mwili wake kuchomwa moto baada ya marehemu kutuhumiwa kuiba kuku wanne ingawa hata hivyo wamiliki wake hawajafahamika.

Tukio hili linakuja siku chache tu baada ya kijana mwingine wilayani Kahama kuuawa na wananchi baada ya kuvamia nyumba ya mtu akiwa na panga na kisu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post