INASIKITISHA !!! KIJANA AFARIKI DUNIA JUU YA MTI SHINYANGA


Mwili wa marehemu George Kwilasa Maswizilo (33)ukiwa juu ya mti unaouona hapo katikati.Ni vigumu kuuona vizuri kwani nguo alizokuwa amevaa zinafanana na mti .Kijana huyo amefariki dunia papo hapo jana saa mbili asubuhi juu ya mti wakati akikata moja ya tawi la  mti huo katika eneo la mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi Mjini shinyang.Unaowaona hapo ni baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo la aina yake 
ambapo marehemu baada ya kukata mti huo ulimwamgukia na kumbana tumboni hali iliyosababisha apoteze maisha yake papo hapo huku akiwa juu ya mti

Mwili wa marehemu ukiwa juu ya mti umebanwa na moja ya tawi la mti aliokuwa anaukata,alikuwa amepewa ujira wa kukata mti huo ikiwa ni ajira inayomwingizia kipato kila siku.Kufuatia tukio hilo mwenyekiti wa mtaa huyo ambaye pia ni diwani wa kata ya Ndembezi bwana David Nkulila kwa kushirikiana na wananzengo wa mtaa huyo walifanya mchango kwa ajili ya gharama za mazishi ya marehemu japokuwa sio mkazi wa mtaa huo(marehemu ni mkazi wa Kitangiri mjini Shinyanga na kazi yake hapo mjini ni kukata miti) na bahati mbaya amepoteza maisha akiwa kazini nje ya eneo alikokuwa anaishi.Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post