Hali Mbaya!!!-MBUNGE WA NYANG'HWALE ATOA MSAADA WA MAGODORO NA VITANDA KUNUSURU KITUO CHA AFYA KALUMWA KATIKA WILAYA MPYA YA NYANG'HWALE MKOANI GEITA



Hatimaye kituo  cha afya Kalumwa kilichopo katika  wilaya mpya ya Nyang’hwale mkoani Geita kimeanza kupata neema ambapo leo kimeahidiwa kupatiwa  magodoro 50 na vitanda 2 vya kujifungulia akina mama vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 3 na laki tano.

Ahadi hiyo imetolewa leo na Mbunge wa Jimbo la  Nyang’hwale mheshimiwa Hussein Nasoro Kassu baada ya kutembelea kituo hicho na kijionea hali halisi ya kituo hicho na kutoa msaada midogo midogo kwa wagonjwa waliolazwa katika kituo hicho vikiwa na thamani ya shilingi laki moja na elfu kumi.

Mbunge juyo amesema  ameamua kutoa misaada na ahadi hiyo ya magodoro 50 na vitanda 2 baada ya kujionea mwenyewe wagonjwa wa jimbo lake wanavyoteseka huku akina mama wakiwa hawana vitanda maalumu vya kujifungulia huku mazingira ya vyoo na mabafu yakiwa machafu.

Aidha kufuatia ziara hiyo ya kushutukiza ya mbunge huyo wa Nyang’hwale ameiomba halmashauri hiyo  kutafuta njia mbadala ya kukisaidia kituo hicho ambacho wagonjwa wake wana hali mbaya huku wakisubiri pesa kutoka serikali kuu.

Naye Mganga mkuu wa kituo hicho DK Nelson Bukuru pamoja na wagonjwa waliokutwa katika kituo hicho wameshukuru sana kwa msaada wa mbunge huyo na kumuomba kuendelea kuwasaidia na kuwaomba wahisani wengine wenye moyo kama wa mbunge kuendelea kukisaidia kituo hicho,


Ziara ya mbunge wa Jimbo la  Nyang’hwale mheshimiwa Hussein Nasoro Kassu katika kituo hicho cha afya imekuja ikiwa ni siku chache tu mtandao huu wa www.malunde1.blogspot.com kuripoti kuhusu hali mbaya katika kituo cha afya cha Kalumwa kilichopo katika wilaya mpya ya Nyang’hwale mkoani Geita.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post