MAANDAMANO YA KUTEMBEA KWA MIGUU KWA KASI KUFANYIKA KESHO MJINI SHINYANGA YAKIONGOZWA NA MKUU WA MKOA ALLY NASSORO RUFUNGA KATIKA SIKU YA KISUKARI DUNIANI

kesho ni zaidi ya hii
Ikiwa kesho ni siku ya kisukari duniani katika mkoa wa Shinyanga maadhimisho ya siku hiyo yataadhimishwa kwa aina yake ambapo kutafanyika maandamano ya kutembea kwa miguu kutoka eneo la hospitali ya mkoa wa Shinyanga kupitia maeneo mbalimbali mjini Shinyanga na kuhitimishwa katika viwanja vya Shy-com ..

Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Dkt Ramadhani Kabala amesema siku ya kisukari duniani hufanyika tarehe 14 mwezi Novemba kila mwaka kwa  lengo la  kuwahamasisha wananchi kujua sababu zinazosababisha  mtu kuwa na ugonjwa wa kisukari na kwa walio na kisukari kuwapa elimu ya namna ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Dkt Kabala mesema katika maadhimisho hayo ya siku ya kisukari  kesho katika mkoa wa Shinyanga,mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga mheshimiwa Ally Nassoro Rufunga ambaye pia ataongoza maandamano ya kutembea kwa miguu

Ameongeza kuwa maadhimisho hayo yataanza kwa maandamano ya kutembea kwa miguu kwa kasi  kuanzia  majira ya saa mbili asubuhi na yataanzia katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga kupitia shule ya Sekondari Buluba iliyoko mjini Shinyanga kuelekea Stendi ya mabasi mjini Shinyanga kupitia eneo la Japanese kona hadi Kanisa la AIC Kambarage baadae Nguzo nane na hatimaye kuishia katika viwanja vya SHY-COM ambapo kiongozi wa maandamano hayo ambaye ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga atatoa hotuba.

Amesema lengo la maandamano ya kutembea kwa miguu kwa kasi ni  kuwahamasisha wananchi kuwa kutembea kwa miguu ni njia bora na rahisi zaidi ya kufanya mazoezi kwa lengo la kukabiliana na ugonjwa wa kisukari na magonjwa mengine sugu yasiyoambukizwa kama vile presha.

Aidha Dkt Kabala amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwani katika viwanja hivyo vya Shy-com pia elimu  itatolewa kwa wananchi  kuhusu namna ya kujikinga na ugonjwa wa kisukari na mambo mbalimbali juu ya ugonjwa huo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post