MSUKUMA AENDELEA KUONESHA UBABE KWA VIONGOZI WA SERIKALI WA MKOA MPYA WA GEITA

Ni katika eneo lenye mgogoro,aliyesimama ni mwekezaji mzalendo aliyejulikana kama Paulo Majaliwa mkazi na mzawa wa wilaya ya Geita anayeendesha mradi wa kuchimba na kusaga mawe na kuuza kokoto
Eneo hilo la Nyantorotoro ambalo mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm mkoani Geita,Joseph Msukuma ametofautiana na serikali ya chama hicho wilayani Geita,baada ya kuwarudisha kwa nguvu wananchi kwenye eneo la mwekezaji lililopo katika kitongoji cha Nyantorotoro mjini Geita ambalo lina mgogoro wa siku nyingi.


Na Valence Robert-Geita.



Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm mkoani Geita,Joseph Msukuma ametofautiana na serikali ya chama hicho wilayani Geita,baada ya kuwarudisha kwa nguvu wananchi kwenye eneo la mwekezaji lililopo katika kitongoji cha Nyantorotoro mjini Geita ambalo lina mgogoro wa siku nyingi.


Mwenyekiti huyo alitoa amri hiyo alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Nyantorotoro ambao baadhi yao ni waathirika wa mgogoro huo unaodaiwa unatokana na baadhi ya wananchi wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa kuchochea ili aondolewe mwekezaji huyo.

Msukuma aliwambia wananchi kuwa warudi kwenye maeneo hayo ambayo mwekezaji tayari ameishasimika mashine za kusaga mawe ili kupata kokoto kwa kutumia nguvu na ubabe.

“Nataka wananchi wote warudi kwenye maeneo yao ya mashamba na muendelee kuchimba mawe na hakuna mtu wa kuwagusa,awe mkuu wa wilaya,awe mkuu wa polisi au mkuu wa mkoa mimi ndo mwenyekiti wa ccm hakuna wa kuwagusa” alisikika huku akishangiliwa na umati wa wananchi waliofika kwenye mkutano huo.




Eneo hilo la Nyantorotoro ambalo mwenyekiti huyo aliagiza wananchi warudi kwenye maeneo hayo linadaiwa kumilikiwa na mwekezaji mzalendo aliyejulikana kama Paulo Majaliwa mkazi na mzawa wa wilaya ya Geita anayeendesha mradi wa kuchimba na kusaga mawe na kuuza kokoto.



Alipoulizwa kuhusu uhalali wa kimiliki eneo hilo mwekezaji huyo,alisikitishwa na kitendo hicho cha mwenyekiti kulazimisha wananchi kurudi katika eneo ambalo anafahamu kwamba linamilikiwa kihalali na mwekezaji .



 “ninamshangaa Musukuma kuongozana na viongozi wa chama cha upinzani (CUF) na kuhamasisha wananchi kurudi kwenye maeneo wanayojua ninayamilki kisheria tangu mwaka jana” alisema mwekezaji.



Aidha,alipoulizwa Afisa madini mkazi wa Geita , Sementa  Haruna  kuhusu mmilki halali wa eneo hilo la Nyantorotoro,alikiri eneo hilo kumilkiwa na Paulo Majaliwa kwamujibu wa sheria ya madini kwa kufuata taratibu zote, “mmilki wa eneo hilo ni bwana Paulo Majaliwa,ana leseni ambayo aliipata kihalali kwa mujibu wa sheria na ofisi yetu ya madini inamtambua kwa namba ya leseni  000229LZ na 000238LZ

 

“Mimi nashangaa kwanini Msukuma haelewani na viongozi wenzake na wakati wote wako chama kimoja na wapo kwa ajili ya kuongoza wananchi wa mkoa wa Geita sasa wananchi wanashindwa waende wafate lipi.maana mwenyekiti anasema na serikali inasema”,alisema Sementa.



Afisa ardhi wa wilaya ya Geita ,Venance Ngeleuya alisema “eneo hilo lilikuwa linamilikiwa na wananchi wa Nyantorotoro Geita ikiwa bado mkoa wa Mwanza,TanRoads walipotaka kusaga kokoto waliwahamisha wananchi hao na kuwalipo fidia wakaondoka,lakini wanasiasa wamekuwa wanawalazisha wananchi kurudi kwenye maeneo hayo na kudai fidia



Aliendelea kusema kuwa wananchi hao walilipwa na TanRoads lakini baada ya mwekezaji(Majaliwa )kumilki eneo hilo na wananchi hao kushawishiwa na wanasiasa kudai fidia mara ya pili,mwekezaji alikubali kuwalipa fidia na hadi sasa wanaomdai ni watu 8 kati ya watu 25 waliokuwa halali katika eneo hilo.



Mkuu wa wilaya ya Geita Manzie Mangochie alipoulizwa kuhusu uhalali wa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(ccm) mkoa wa Geita kutoa amri ya kurudisha wananchi katika eneo la mwekezaji,alisema.



 “ninashangaa mwenyekiti wa chama mamlaka ya kutoa amri ya kurudisha wananchi hao ameitoa wapi na ametumia sheria ipi”



“ Ninachojua kuna taratibu za kisheria zinazotakiwa kufuatwa lakini kwenye taratibu hizo mwenyekiti wa chama hana nafasi ya kufanya hayo aliyo yafanya,yuko kinyume cha taratibu za kisheria” alisema Mangochie.

 

,Mimi kama mkuu wa wilaya naomba wananchi wafuate sheria wasidanganywe na wanasiasa wanapotoshwa kabisa kwani sheria iko pale pale na zitafuatwa na kuzingatiwa.



Agizo hilo la mwenyekiti huyo  wa ccm mkoa wa Geita limekuja ikiwa ni zaidi ya  mara tatu akitoa maagizo yanayoashiria kuvunja sheria za nchi huku akiwaambia wananchi wanaweza kufanya lolote ilimradi wameagizwa na kiongozi  huyo wa ccm.



Baadhi ya maagizo aliyowahi kutoa kwa wananchi katika mkoa wa Geita ni pamoja na kuwazuia wasifanye usafi katika mji wa Geita kila Alhamis kama ilivyokuwa imeamriwa na kamati ya Afya ya wilaya,kuzuia maafisa mistu wasikamate watu wanaokata miti na wachoma mkaa na hivi karibu aliwaambia wananchi wa Bukombe kurudi kwenye pori walikokuwa wamehamishwa na serikali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post