GARI LA UHAMIAJI MKOA WA GEITA LATUMIKA KUUIBIA MGODI WA GEITA,LATOROSHWA POLISI KIMYA KIMYA, HALI YAWA TETE KWA WAANDISHI ,WANUSURIKA KUPIGWA

Ikiwa ni siku chache baada ya gari la kubebea wagonjwa la kituo cha afya cha Nzera katika halmashauri ya wilaya ya Geita kukamatwa mgodini likiwa na mapipa mawili ya mafuta mali ya mgodi wa Geita Gold Mine,hali katika hali iliyoacha watu wengi midomo wazi, hali hiyo imejirudia katika staili ya namna yake  ambapo gari la ofisi ya  uhamiaji mkoani Geita limekamatwa katika  mgodi huo wa  [GGM] likiwa na dizeli pamoja na kiroba cha mchanga.

Tukio hilo limetokea saa 2.30  baada ya walinzi  wa mgodi kulitilia mashaka na kulazimika kulisimamisha  kwa ajili ya upekuzi na kukuta mapipa ya dizeli na kiroba hicho ndani ya gari hilo lenye namba za usajili T.690 AKW lililokuwa likiendeshwa na koplo Anorld.


 Aidha  baada ya gari hilo kukamatwa gari hilo lilipelekwa katika kituo cha polisi cha Geita na baada ya hapo likahamishiwa ofisi ya uhamiaji.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa geita Bi Purudensia  Poltas alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa Gari hilo alisema hana taarifa zozote na kwamba yeye hakuwepo alikuwa safarini


Naye afisa habari wa Mgodi wa GGM bwana Tenga Bill Tenga amesema kuwa Gari hilo limekamatwa likiwa na kiroba cha mchanga Spana za aina mbalimbali pamoja dizeli madumu madumu mawili ili vyote vikiwa ni mali za mgodi huo.


 Afisa uhamiaji wa mkoa wa Geita Bw Charles Washima alipotakiwa kujibu juu ya tuhuma za gari hilo kukamatwa mgoini alisema kuwa gari hilo lilikuwa limepelekwa kwa matengenezo na kwamba vifaa hivyo vilisahaulika ikiwa ni spana na lita saba za oil tu.
  
Taarifa za gari hilo ni kuwa awali lilikuwa mali ya mgodi wa Geita Gold Mine kabla ya kupewa ofisi ya uhamiaji mkoa wa Geita,na katika hali isiyokuwa ya kawaida mwandishi wa habari hii bwana Valence Robert alipewa vitisho na kunusurika kupigwa na mmoja wa watumishi wa ofisi ya uhamiaji mara baada ya kugundua kuwa ameenda kuandika habari hiyo.


Na Valence Robert-Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post