MKUTANO WA CHAMA CHA MAJAJI NCHINI ( JMAT ) KUFANYIKA KESHO MKOANI GEITA,HOJA KIBAO KUJADILIWA


Mkutano wa siku moja wa majaji wa nne (4) pamoja na mahakimu  kutoka mkoa wa mwanza na Geita wa kujadili  jinsi ya kuendesha kesi mbalimbali unatarajia kufanyika kesho tarehe 07/12/2013 mkoani Geita

Akiongea na vyombo vyambo vya habari ofisini kwake Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya Geita Bw.DEUS KAMUGISHA ambaye atakuwa ni mwenyeji wa kutano huo amesema  mkutano huo utaanza kesho saa tatu asubuhi na utafanyika katika Ukumbi wa Alfendo Hoteli ulioko mjini Geita


Ameongeza kuwa katika mkutano huo mgeni rasmi atakuwa Mkuu wa mkoa Geita Bwana Magarura Said Magarura katika mkutano huo pamoja na kujadili jinsi ya kuendesha kesi kutakuwepo na hoja mbili ambazo zitawasilishwa na majaji 2 ambazo ni UENDESHAJI WA KESI ZA MILATHI itakayowasilishwa na ANM SUMARI ambaye ni jaji mfawidhi mahakama kuu kanda ya mwanza ya pili UENDESHAJI WA KESI ZA NDOA NA TARAKA ambayo itawasilishwa na S.MWANGES Jaji mahakama kuu kanda ya mwanza ambazo zote zitajadiliwa katika mkutano huu

Bw.Kamugisha amesema japo majaji hao watawasilisha hoja hizo lakini watakuwepo majaji wengine wawili ambao ni Z.MERO Jaji mahakama kuu ya mwanza na Bw. Bukuku Jaji Mkuu Mahakama Kanda ya mwanza

Na mahakimu wa wilaya zote za mkoa wa mwanza lakini katika mkoa wa Geita zitashirikishwa wilaya 2 ambazo ni Geita Mjini na Nyagh’wale hizo ndiyo wilaya zitakazo shiriki katika mkutano huo.


Wanachama  hao wa chama kinachojulikana kwa jina la JMAT

                                           (Judges' and Magistrates' Association Tanzania )

ambapo mwenyekiti wake Bw.France Mwasiga ambaye ni mwenyekiti wa Tawi hilo atahudhulia mkutano huo  
Na Valence Robert-Geita  

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post