Hatari!!! WANAWAKE WAOGA KUTUMIA KONDOMU


Na Ali Lityawi- Kahama

Sababu ya wanawake kuongoza kwa maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) inatokana na kukosa maamuzi juu ya kutumia kinga kama kondom wanapofanya tendo la ndoa.
Hayo yalibainishwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga jana na Mwezeshaji Kaskile Jumanne katika semina iliyoandaliwa na Shirika la The Foundation for Human Health Society (HUHESO) inayotekeleza mradi wa kuwakomboa wasichana wanaofanya biashara ya ngono, unaofadhiliwa na Rapid Funding Envelop (RFE) ya jijini Dar es Salaam.
Jumanne ambaye ni Daktari wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama, alisema wanawake huathiriwa na mfumo dume wa kukosa maamuzi katika tendo la ndoa jambo ambalo huchangia wakipata maambukizi kwa urahisi.
Alibainisha kuwa kwa jamii ambayo ni muumini mzuri wa kutumia kondomu lakini baadhi ya watu pia hujikuta wakipata maambukizi mapya kutokana na kutofahamu matumizi sahihi wakati wa kuvaa, kuivua na kuhifadhi baada ya matumizi.
Mkurugenzi wa HUHESO, Juma Mwesigwa alisema wanawake wanapaswa kubadilika na kuondokana na jukumu la mapenzi kutawaliwa na mwanaume ili kuondokana na hatari ya kupata maambukizi mapya.
Mwesigwa alisema wanawake hawana budi kujitambua kwa kubadilika na kuwa jasiri jambo litakalosaidia kupunguza maambukizi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post