Kumbe Inawezekana!! MAHAKIMU NA MAJAJI WATAKIWA KUACHA KULUNDIKA MAFAILI YAWATUHUMIWA



Mahakimu na majaji  wa mikoa ya Mwanza na Geita wameaswa kuendelea kuhukumu kesi za wananchi wa mikoa hiyo bila kujali masikini au tajiri,na kuacha kulundika mafaili ya watuhumiwa,kama ilivyo hivi sasa.

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Geita Bwana Magarura Said Magarura  kwenye mkutano wa chama cha majaji [4]  pamoja na mahakimu zaidi ya sabini kinachojulikana kwa jina la[JMAT] waliotoka  mikoa ya Mwanza na Geita ambao umefanyika jana Jumamosi  katika ukumbi wa Alifendo Hotel ulioko mjini Geita.

Mkutano huo uliokuwa na lengo la kutatua migogoro ya ndoa pamoja na mirathi.

 Magarura amesema japokuwa  kuna mahakimu wanawatendea haki wananchi lakini kuna baadhi ya mahakimu wanafanya kazi kwa kuangalia uwezo wa mtu kama ni tajiri au masikini hivyo kama wapo wanaowanyima haki wananchi basi waache tabia hiyo mara na wasipoacha watachukuliwa hatua kali kwani kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu kutotendewa haki kwenye kesi zao na mahakimu.

 Magarura ameongeza kuwa majaji hao pamoja na mahakimu wanatakiwa kutumia mkutano huo kujifunza na kuachana na mapungufu wanayokabiliana nayo ikiwa ni pamoja na kuendelea kuhukumu kesi za wananchi kwa haki.

 Naye A.N,M Sumari ambaye ni jaji mfawidhi Mahakama ya kanda ya Mwanza  alimshukuru mkuu wa mkoa wa Geita kwa kukubali kuwa mgeni rasmi na kuahidi kuyafanyia kazi yote yaliyosemwa na mkuu huyo na kuahidi kuwachukulia hatua kali baadhi ya mahakimu wanaojihusisha na Rushwa kwenye mahakama mbalimbali za kanda ya Mwanza.


Bi Sumari ameongeza kuwa pamoja na hayo kumekuwa na changamoto mbali mbali zizowakabili ikiwa ni pamoja na kukoa ofisi na vitendea kazi vichache  kwenye mahakama mbali mbali za kanda ya Mwanza na Geita na kumuomba kuwasaidia pale wanapokuwa na shida.
Na Valence Robert -Geita 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post