Kahama kwanuka tenaaa! MAJAMBAZI MENGINE YAUAWA KWA RISASI WAKATI YAKIJIANDAA KUVAMIA MGODI WA DHAHABU



Majambazi  watatu wameuawa wakati wakirushiana risasi na polisi wakati majambazi hayo yakiwa katika harakati za kuvamia mgodi wa dhahabu wa  Bulyanhulu uliopo wilayani Kahama usiku wa kuamkia leo.

Kamanda wa polisi mkoa wa  Shinyanga SACP Evarist Mangala amesema tukio hilo limetokea  majira ya saa sita usiku katika  kijiji Namba Tisa,kata ya Bulyanhulu ambapo watu hao wasiofahamika jina wala makazi yao umri kati ya 25-30 walikuwa wanajiandaa kuvamia mgodi


Kamanda Mangala amesema majambazi hayo yalikuwa na mabomu matatu ya kurusha kwa mikono, bunduki aina ya SMG  mbili na risasi 94.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post