Kahama Kumenuka!!! MAJAMBAZI MATANO YADAKWA BAADA YA KUVAMIA

Picha ya jambazi lililouawa kwa risasi baada ya kuvamia hivi karibuni huko Kahama
Watu watano wanaodaiwa kuwa ni majambazi wnashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga muda mchache tu baada ya kuvamia duka la mfanyabiashara mmoja na baadaye kuvamia nyumba ya mfanyabiashara mwingine katika kijiji hicho.

Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa mbili usiku ambapo majambazi hao walimvamia Mussa Bernard Bugani(38) mfanyabiashara na mkazi wa kijiji hicho akiwa dukani kwake na kupora pesa,vocha za simu.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Kihenya Kihenya amesema baada mkali uliendeshwa na wananchi kwa kushirikiana na waya tukio hilo jeshi la polisi na wananchi wa kijiji cha Lunguya na kufanikiwa kukamata majambazi hao pamoja na bunduki moja aina ya SMG yenye namba za usajili UA-42571997 na risasi 26.


Kamanda Kihenya amewataja majambazi hao kuwa ni  Bakari Ramadhani Lumala(31),mfanyabiashara,AmonLubisi(24),mfanyabiashara,Emmanuel Petro Charles(20) wakala wa Airtel Money,Pius Ernest Samson(34) mkulima pamoja na Silas Iselubisi(25) mkulima wote wakazi wa  Segese  wilayani Kahama.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post