MEYA APIGWA RISASI MAENEO YA AIRPOT

6063
Ukol Talumpa enzi za uhai wake
Sasa hivi matukio ya watu kupigwa risasi kwenye mikasa ambayo sio ya kawaida sio Tanzania tu bali hata kwenye nchi nyingine au maeneo mengine ambayo hayakuwahi kuwa na rekodi za ukatili wa aina hii.

Taarifa ya leo inamuhusu Meya wa mji wa Labangan  nchini Philippine ambaye amepigwa risasi akiwa na watu wengine watatu maeneo ya airport huko Manila Philippine ambapo Ukol Talumpa imeripotiwa alipigwa risasi pamoja na mke wake, mtoto wao wa miezi 18 na mtu mwingine mmoja na kufariki dunia.

Ripoti hii inasema watu wengine wanne wamejeruhiwa kwenye tukio hilo wakati mshambuliaji huyo alipotekeleza shambulio hilo huku kiongozi huyo aliekuwa nje ya terminal 3 ya Airport akisubiri usafiri ambapo ndio mtu mmoja akiwa kwenye pikipiki alipita na kufyetua risasi kwa karibu na kukimbia na pikipiki yake.

Chanzo cha tukio hili bado hakijajulikana.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post