Hatari!!!MAJAMBAZI MAWILI YAUAWA WAKATI YAKIRUSHIANA RISASI NA POLISI MKOANI SINGIDA,...TUNAOMBA RADHI KWA PICHA UTAKAZOZIONA HAPA CHINI


Mwili wa moja ya majambazi yaliuawa mkoani Singida ukiwa katika hospitali ya mkoa huo

 Mwili wa jambazi jingine lililouawa Singida

Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555  iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida


Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555  iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida

Jeshi  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea Desemba 9 mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida.

Amesema watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya uhalifu.

Akielezea zaidi kuhusu tukio hilo, amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zililifikia jeshi la polisi na ndipo askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.

“Baada ya polisi kufika kijijini hapo watu hao walishtuka kuwa wanafuatiliwa na askari polisi na hivyo kuanza kukimbia kuelekea kijiji cha Uhamaka kwa kutumia pikipiki yenye namba za usajili T. 634 BTW aina ya Sanlag yenye rangi nyeusi”,amesema Kamwela.

“Hali ilipokuwa ngumu zaidi, walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi nao ikwabidi kujibu mapigo na katika majibizano hayo ya risasi, majambazi mawili yaliweza kujeruhiwa huku mmoja akifanikiwa kutoroka",aliongeza.

Amesema majambazi hayo yaliyojeruhiwa yalifariki dunia njiani wakati yanakimbizwa katika hospitali ya mkoa kwa matibabu.

Amesema katika eneo la tukio, ilipatikana bunduki moja aina ya SMG yenye namba 34555 ikiwa na risasi saba kwenye magazine.  Pia pikipiki iliyokuwa inatumiwa na majambazi hayo na ilipatikana.

Kamwela ametoa wito kwa wananchi kuendelea na moyo huo huo wa kuwafichua watu wanaowatilia shaka ili waweze kudhibitiwa mapema kabla ya kufanya uhalifu.


Chanzo-Chami wa Matukio blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post