Wakulima wa Pamba wawasha moto !!!! WATAKA PIA WAZIRI CHIZA AWAJIBISHWE,FUATILIA ZAIDI HAPA IMEKUWAJE......

Rais Kikwete

                                       Waziri Chiza

Baada ya Rais Kikwete kutengua uteuzi wake kwa mawaziri wa mambo ya ndani ya nchi, maliasili na utalii, ulinzi na mifugo na uvuvi ,wakulima wa zao la pamba mikoa ya Shinyanga na wamemwomba Mheshimiwa rais kumwajibisha pia  kwa waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandishi Christopher Chiza.


Wakulimahao wamesema Chiza hana budi kuwajibishwa kutokana na kitendo chake cha  kuruhusu matumizi ya mbegu za pamba zinazosambazwa na kampuni ya Quton,zisozokuwa na manyoya ambazo zimegoma kuota katika maeneo mengi katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Geita na Simiyu na kusababisha hasara kwa wakulima hao na hawalipwi fidia kutokana na hasara hiyo.

Naye katibu  wa Chama cha wakulima wa zao la pamba wilayani Kahama (TACOGA), Paulo Ntelya amesema waziri Chiza ni mmoja wa mawaziri waliolalamikiwa na wakulima wa zao la korosho wakati wa ziara ya katibu mkuu wa CCM Taifa, Abdurahman Kinana alipokuwa katika ziara ya mikoa ya kusini na kwamba hata CCM wenyewe walipendekeza waziri huyo awajibishwe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post