HAWA NDIYO WAIGIZAJI MATAJIRI ZAIDI DUNIANI


Screen Shot 2014-05-23 at 9.40.55 AMWapenzi wengi wa filamu duniani watakuwa wanalitambua jina lake ambapo kwa Tanzania ni maarufu zaidi uswahilini lakini duniani ndio anatajwa kuwa muigizaji anayejulikana zaidi.

 Jina lake ni Shahrukh Khan ambae ni mwigizaji wa filamu kutoka India ambapo jana ametengeneza headlines baada ya kutajwa na jarida la maswala ya fedha la Wealth-X la Singapore ndio mwigizaji tajiri zaidi Asia pia anashika nafasi ya pili duniani nyuma ya comedian Jerry Seinfeld ambaye ana utajiri wa dola za kimarekani milioni 820.

Jerry Seinfeld
Jerry Seinfeld
Khan ambaye ni maarufu kwa jina la Kingh Khan ana utajiri wa $600m akiwa kawazidi waigizaji wakubwa Hollywood kama Tom Cruise mwenye $480 million, akiwafuatia na Johny Depp na Tyler Perry ambao wote wana $450 million. srk-tom-johnny 

Listi hiyo imechanganya waigizaji washindi wa tuzo za Academy kama Jack Nicholson ($400 million), Tom Hanks ($390 million) na Clint Eastwood ($370 million) Nicholson ni namba 6 akifuatiwa na Hanks, Bill Cosby, Eastwood na Adam Sandler.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم