MWANAMKE KIKONGWE AUAWA KWA KUCHARANGWA MAPANGA

Matukio ya vikongwe kuuawa kwa kucharangwa mapanga mkoani Geita yameendelea kushika kasi ambapo 
mwanamke aitwaye Mariam Kidesheni(60) mkazi wa kijiji cha Isamilo kata ya Kamhanga wilayani Geita ameuawa na watu wasiofahamika kwa kukatwa mapanga.

Tukio hilo limetokea Me 25 mwaka huu saa 2 usiku ambapo inadaiwa kuwa mama  huyo  baada ya kumaliza kula chakula cha usiku alivamiwa na watu wasiofahamika 
wakiwa na mapanga kisha kuanza kumkata kata sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo kichwani,shingoni na sikioni hadi kufa.

Diwani wa kata ya Kamhanga Dionizi Bugali na Kamanda wa polisi mkoani Geita Joseph Konyo wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Na Valence Robert wa Malunde1 blog-Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم