Pombe noma sana!!!KIJANA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUBUGIA VIROBA VYA ZED KUPITA KIASI HUKO KATAVI


Mkazi wa Kijiji cha Ibindi, Tarafa ya Nsimbo, wilayani Mlele, Michael Silanda (26), amefariki dunia baada ya kunywa pombe za viroba aina ya Zed kupita kiasi bila kula.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, alisema tukio hilo lilitokea Mei 5 mwaka huu, saa 6 usiku  kijijini  hapo.

Alisema siku ya tukio, Silanda alikwenda baa na kuanza kunywa pombe hiyo bila kula kitu chochote hadi saa 6 usiku alipoamua kurudi nyumbani kwake huku akiwa amelewa kupita kiasi.

“Baada ya kufika nyumbani kwake aliingia ndani na kulala bila kula na siku iliyofuata saa 2 asubuhi ndipo  walipomkuta akiwa amefariki dunia,” alisema.

Kamanda Kidavashari alisema uchunguzi wa awali umebaini kifo hicho kimesababishwa   na Silanda kunywa pombe kupita kiasi bila kula  chakula.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa kufanyiwa uchunguzi na utakapokamilika watakabidhiwa ndugu kwa mazishi.


Na Walter Mnguluchuma

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post