RAIS HOSNI MUBARAK AHUKUMIWA KIFUNGO JELA MIAKA MITATU

Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri, Hosni Mubarak amehukumiwa jela miaka mitatu.
Wanawe wawili Alaa na Gamal wamepata kifungo cha miaka minne kila mmoja.
Wendesha mashitaka walisema kuwa wanawe Mubarak waliponda mamilioni ya dola pesa za umma zilizotengewa kukarabati ikulu ya Rais na badala yake wakafanyia ukarabati nyumba zao za kifahari.
Wametakiwa kulipa pesa hizo za serikali na kutozwa faini ya dola milioni tatu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم