TAZAMA PICHA UONE JINSI ASKOFU GERVAS NYAISONGA ALIVYOWASILI KWENYE JIMBO LAKE JIPYA LA MPANDA

Askofu Gervas Nyaisonga wa jimbo la Katoliki la Mpanda akisalimiana na Mapadri wa jimbo hilo katika eneo la mto koga Hapo jana ambapo ndipo linapoanzia Jimbo katoliki la Mpanda wakati alipokuwa akiwasili rasmi kwenye jimbo lake jipya la Mpanda akiwa anatokea jimbo la Dodoma 
Askari wa skauti wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda wakiwa katika eneo la daraja la mto koga wakimpokea askofu Gervas Nyaisonga alipowasili hapo jana akitokea jimbo la Dodoma ambapo askofu Nyaisonga alipokuwa analiongoza kabla ya kuhamishiwa Jimbo la Mpanda na amesimikwa jana kuwa askofu wa Jimbo la Mpanda

Askofu Gervas Nyaisonga wa Jimbo katoliki la Mpanda akibusu Ardhi hapo jana katika kijiji cha Kamsisi ikiwa ni ishara ya kuhamia rasmi kuliongoza jimbo la Mpanda akitokea jimbo katoliki la Dodoma
Msafara wa waendesha pikipiki wakiwa katika eneo la uwanja wa ndege mjini Mpanda wakiwa wanaongoza msafara wa kumpokea askofu Gervas Nyaisonga hapo jana ambae amehamishiwa jimbo la Mpanda akitokea jimbo la dodoma
Mapadri wa kanisa katoliki wakiwa kwenye kanisa kuu la jimbo Katoliki la Mpanda kabla ya kuanza kwa ibada ya kukabidhiwa ufunguo wa kanisa hilo askofu Gervas Nyaisonga ambae amehamishiwa jimbo la Mpanda ikiwa ni ishara ya kuyaongoza makanisa na kuyasimamia makanisa yote ya jimbo katoliki la Mpanda 

Picha zote na Walter Nguluchuma 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post