Ukawa Noma!! DR SLAA ADAI KINANA NI MUONGO,MNAFIKI KWA SABABU ANATAKA SERIKALI 2 ILI YEYE NA MAFISADI WAENDELEE KUIBA RASILIMALI ZA WATANZANIA

Katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) ambaye ni kiongozi wa timu ya ukawa ukanda wa kaskazini na kanda  ya ziwa,Dr.Willbrod  Slaa akizungumza mjini Geita
Katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) ambaye ni kiongozi wa timu ya ukawa ukanda wa kaskazini na kanda  ya ziwa,Dr.Willbrod  Slaa amesema katibu mkuu wa chama cha mapinduzi (ccm)Abdulrahaman Kinana anataka mfumo wa serikali mbili ili yeye na mafisadi waendelee kuiba rasilimali za watanzania.

Dr.Slaa alisema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya magereza mjini Geita wakati akifafanua hoja mbalimbali zilizowafanya wajumbe wa bunge maalum la katiba mpya kutoka nje ya ukumbi wa bunge kwa umoja wao unaojulikana kwa jina la  Ukawa.

Dr Slaa alifafanua kuwa,Kinana amekuwa akiwadanganya watanzania kuwa katiba mpya sio muarobaini wa matatizo ya Watanzania na akijua fika kwamba haki za wananchi zinapatikana kwenye katiba yenyewe.

“Kinana amekuwa akipotosha watanzania,anawaambia eti katiba mpya sio muarobaini wa matatizo yao,lakini anawadanganya,ni muongo,ni mnafiki wa hatari sana na vitabu vitakatifu vinasema yeyote anayepotosha walio wadogo anastahili kufungiwa jiwe shingoni na kutupwa baharini”,alisema Dr Slaa.

“Haki zote za msingi za binadamu zinazomlinda na kumtetea mwananchi wa kawaida lazima zipatikane kwenye katiba na ziwekewe masharti ya kuziheshimu ili zitendeke na ndiyo maana Afrika ya kusini mwaka  jana wananchi walipeleka kesi mahakamani na imeruhusiwa mwananchi wa Afrika kusini asipotibiwa  anashtaki serikali lakini kwa Tanzania usipopata Maji,elimu au matibabu huwezi kuishtaki serikali”,aliongeza.

Alisema kuwa, Kinana anapigana kufa na kupona akitetea serikali mbili kwa sababu serikali mbili zinaruhusu mafisadi waendelee kuiba mali za watanzania bila kuwajibishwa na mamlaka zilizopo.

Alitolea mfano kuwa Meli inayomilikiwa na Kinana ilikamatwa baharini ikiwa imesheheni meno  ya tembo  yenye uzito takribani 2000 yenye thamani zaidi ya bilioni 5 ikielekea Hong Kong lakini hadi leo hii Kinana hajachukuliwa hatua yoyote.

“Ndugu zangu mfumo wa serikali tatu unazuia ufisadi wa rasilimali za wananchi zisiibiwe na kuchezewa na mafisadi na ndiyo maana ccm na Kinana wanazunguka nchi nzima wanahubiri serikali mbili ili waendelee kupata mianya ya kuiba Tembo na madini yetu bila kuchukuliwa hatua” alisema

  Mkutano huo wa Ukawa uliohitimisha awamu ya kwanza ya ziara ya viongozi hao,ulihutubiwa pia na viongozi wengine wa kutoka chama cha wananchi (cuf) na NCCR-Mageuzi.

Na Valence Robert wa Malunde1 blog-Geita
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post