FIFA 2014 BRAZIL: MECHI KUBWA YA LEO ENGLAND VS ITALY

Siku ya tatu ya michuano ya kombe la dunia inaanza baadaye hii leo huku mechi inayongojewa kwa hamu na mashabiki wengi wa soka ikiwa ile ya Uingereza dhidi ya Italy.

Timu hizo za bara Ulaya zitakutana katika uwanja wa mji wa Manaus katikati ya msitu wa Amazon.

Katika mechi nyengine Colombia itakabiliana na Ugiriki huku Uruguay nayo ikichuana na Costa Rica.

Hapo jana miamba ya soka duniani ambayo ndio bingwa mtetezi wa kombe la dunia Uhispania, ilipata kichapo cha mabao matano dhidi ya Uholanzi katika mechi ya kusisimua iliotawaliwa na Uholanzi.

Vilevile Mexico iliibwaga Cameroon kwa bao moja kwa bila kabla ya Chile kuichapa Australia mabao matatu kwa bila.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post