Maombi mazito!!! KANISA LAENDESHA MAOMBI KUWAOMBEA WASANII WA BONGO MUVI WASIENDELEE KUFA,TAZAMA PICHA HAPA

Mwakifwamba na Dotnana wakiwa wamezama katika neno.
Mwakifwamba (wa pili kushoto) akiwa katika nguvu ya maombi.
Mchungaji Kiongozi Harris Kapiga akiendesha maombi.

Simon Mwakifwamba, Bahati Bukuku na Dotnata wakicheza wimbo wa Dunia Haina Huruma ulioimbwa na Bahati Bukuku.

Mapepo nayo yalifunguka kwa dada huyu baada ya maombi.

Maombi yakiendelea.
Mwakifwamba akiwa katika maombi

Moja ya mabango yaliyokuwa kanisani.Mwimbaji Bahati Bukuku akiwa katika red carpet.
Huyu ni Mchungaji Mbeyela ambaye ni mume wa mwibaji Upendo Nkone.Mchungaji Harris Kapiga akiwaombea watoto katika siku ya kuzaliwa mtoto wa kiume (aliyevaa kofia).Waimbaji wa kwaya wakiongoza maombi.
Kijana mpiga ngoma (drums) wa kundi la kwaya akifanya kazi yake kwa ufasaha.Mtaalamu wa kucharaza kinanda.
‘’MATESO basi, damu ya Yesu yatosha’’.  Hiyo ni kaulimbiu ya leo iliyotolewa katika Kanisa la Nchi ya Ahadi lililopo Sinza-Kamanyola jijini Dar, chini ya Mchungaji Kiongozi Harris Kapiga, wakati wa maombi maalumu kwa ajili ya wasanii wa Bongo Muvi ili kuvunja roho ya mauti juu ya tasnia hiyo ya filamu ambayo imewakumba wasanii wake. 

Maombi hayo pia yalikuwa ni kuwaombea ulinzi wote waliomo na wanaotamani kuingia katika tasnia hiyo.

Maombi hayo yaliwakilishwa na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Saimon Mwakifwamba, wasanii na waimbaji Bahati Bukuku, Dotnata na wengineo.

(Na Gabriel Ng’osha, Shani Ramadhani na Chande Abdalah / GPL)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post