DABI YA SHINYANGA KURINDIMA KESHO KATIKA DIMBA LA CCM KAMBARAGE MJINI SHINYANGA


Stand Fc
Mwadui FC
Waswahili wanasema mafahari wawili wakikutana kinachoumia ni nyasi ndivyo ambavyo itakuwa siku ya kesho katika mchezo wa kirafiki baina ya mahasimu wawili katika Soka la Shinyanga baina ya Stand United Fc dhidi ya Mwadui fc mchezo utakaopigwa katika uwanja wa ccm Kambarage mjini Shinyanga kuanzia saa kumi jioni.

Ikumbukwe timu hizi zilikuwa katika kundi moja mwaka jana katika ligi daraja la kwanza Tanzania bara,hivyo mchezo wa kesho utakuwa ni mkali na wa kusisimua kwani timu zote zina vikosi vizuri na zimefanya usajili katika dirisha dogo.

Na Kadama Malunde-Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post