Geita Kunani? BIBI NA MJUKUU WAUAWA KWA MAPANGA NA WATU WALIOVAA NGUO NYEUSI

Pichani ni  Seleman Mlela mwenye umri wa miaka 75 mkazi wa Nyarugusu Wilayani Geita Mkoani Geita akiwa anauguza majeraha katika hospitali ya Wilaya Geita baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake wiki iliyopita kisha  kucharangwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kwenye paji lake la uso-Picha  na Valence Robert-Malunde1 blog Geita.

Mfanyabiashara  wa nafaka mjini  Katoro  wilayani  Geita  Mkoani  Geita   Tatu  Leonard (40)  pamoja  na   Bibi  yake  Kabula   Masunga (80) wameuawa  kikatili  kwa  kucharangwa  mapanga na watu wasiofahamika  huku  Anastazia   Manogoleku (60) ambaye ni  Mama  yake  mzazi akilazwa  katika  hospitali  ya wilaya  ya  Geita  kwa  aajili ya   matibabu  zaidi   baada  ya kujeruhiwa  vibaya  na watu  hao.

Kwamujibu  wa  Diwani  wa  kata  ya   Katoro  Gervas  Daud  Kabulu  alisema   kuwa  tukio hilo  la  kinyama  limetokea   katika  kitongoji  cha Ludete mjini  Katoro  majira ya saa mbili usiku wa kuamkia  esemba 19  mwaka  huu  wakati  wanafamilia  hao  wakipata chakula cha usiku .

Kabulu  alisema   kuwa   watu zaidi  ya wawili    wasiofahamika  wakiwa  wamevalia  nguo  nyeusi  usoni  kwa  lengo  lakuficha  sura  zao  walifika katika  familia  hiyo  na kisha kuanza  kuwashambulia  kwa  mapanga  bila  huruma  na kisha  kutokomea  kusikojulikana.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Geita Dkt Adamu
Sijaona amewataja waliofariki dunia kuwa ni Tatu Leonard(40) Kabula Masunga(80) na kwambaTatu alifikishwa hospitalini akiwa amefariki na  Kabula alifariki juzi asubuhi.

Dkt Sijaona watu hao walikuwa wamekatwa mapanga sehemu za kichwani na shingoni hali iyosababisha vifo vyao.

Amesema katika tukio hilo Anastazia Manogoleku(60) amejeruhiwa kichwani na kidole gumba cha mkono wa kushoto na hali yake inaendelea na matibabu katika hospitali ya wilaya ya Geita.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Joseph Konyo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo  na kuongeza kuwa uchunguzi unafanyika ili  kufahamu chanzo cha mauaji hayo na kuwakamata wale wote waliohusika na tukio hilo na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Na Valence Robert-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post