UMEISIKIA HII YA VIJANA WALIOTAKA KUIBA SANAMU LA BIKIRA MARIA KANISANI? IKO HAPA

 http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/12/Mar.jpg
Vijana watatu mkoani Songea wametakiwa kwenda na wazazi wao kutubu dhambi za kutaka kuiba sanamu la Bikira Maria katika Kanisa Katoliki la Kigango cha Samora. 


Katekista wa Kigango hicho Keneth Mhagama alisema vijana hao walifanya jaribio hilo usiku wa manane baada ya ibada ya mkesha ambapo walinzi walifanikiwa kuwadhibiti kabla hawajafanikiwa na wakawekwa mbaroni.

Vijana hao ni Ahmed, Mohammed na Leonard ambapo Padri wa Kanisa hilo Cristom Kapinga amesema vijana hao wanatakiwa kutubu la sivyo watawaacha kwenye mikono ya sheria washughulikiwe.
Chanzo cha Habari: Gazeti Mtanzania, December 26.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post