YULE NABII ALIYETABIRI MWISHO WA DUNIA AFARIKI DUNIA

 
Kiongozi wa kanisa la house of Yahweh nchini kenya aliyetabiri mwisho wa dunia mwaka 2006 amefariki dunia.

Kiongozi mmoja wa dini ambaye alipata umaarufu nchini Kenya kwa kutabiri mwisho wa dunia mwaka 2006 amezikwa katika kijiji cha Bomet.

Kiongozi huyo wa madhehebu ya House of Yahweh Willy Kiplangat Sang alizikwa masaa machache baada ya kifo chake katika shamba la babaake kijijini Matarmat katika sherehe iliohudhuriwa na jamii yake ,majirani na wafuasi wa kanisa hilo.

Ndugu za nabii huyo aliyezingirwa na utata wanasema aliugua ugonjwa wa kifua kikuu nyumbani mwake huko Mauche kaunti ya Nakuru ambapo alikuwa mkulima na muhubiri.
via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post