BILL GATES SASA ANAKUJA NA MRADI WA MAJI YANAYOTOKANA NA KINYESI CHA BINADAMU

gate
Mmiliki wa kampuni ya Microsoft Corporation, Bill Gates ameendelea kuuthibitishia ulimwengu kwamba haogopi kuwekeza pesa yake kwenye biashara yoyote Duniani.

Ni mmoja ya watu wanaofadhili miradi mikubwa ya kilimo Afrika, leo kuna hii story ambayo kama ingekuwa Bongo mtu anawekeza upande huu ni wachache ambao wangemuunga mkono.
Picha na video zimeenea mitandaoni, Gates kaamua kugeukia huu mradi wa maji safi ya kunywa ambayo yametengenezwa kutokana na kinyesi cha binadamu.
Mikakati ya Gates ni kushirikiana na Kampuni hiyo kusambaza mitambo hiyo katika nchi mbalimbali maskini ikiwemo Senegal muda mfupi baada ya majaribio yake kukamilika.
Teknolojia hiyo imeungwa mkono na shirika la WaterAid ambalo limesema kuwa litasaidia sana katika maeneo ya mengi yenye ukame ambapo kulingana na shirika hilo watu millioni 748 hawana maji safi ya kunywa.
human
Video iliyowekwa katika blog yake, Bill Gates alishuhudia hatua zote, kuanzia kinyesi cha binadamu kikiingizwa katika mtambo huo mpaka maji yalipotoka na akayanywa baada ya kupitia hatua zote za utayarishaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post