Gazeti la Charlie Hebdo leo limeanza
kusambaza toleo la gazeti lake ambalo limechapishwa kibonzo cha Mtume
Mohammad kwenye ukurasa wake wa mbele.
Nakala Milioni za gazeti hilo zimeanza kusambazwa na nyingine zitafuata iwapo wanunuzi wataongezeka.
Picha ya kibonzo hicho iliyopo ukurasa mbele wa gazeti hilo inamwonyesha Mtume Mohammad akilia.
Wachambuzi wa mambo wanaona kuwa picha hiyo itachochea chuki.
Hata
hivyo waandishi wa habari wa gazeti hilo wanasema ukurasa wa mbele
unamaanisha Waandishi wa habari wamewasamehe waliotekeleza shambulizi la
kigaidi lililofanyika Jumatano wiki iliyopita.
Naibu Mhariri wa
Gazeti la Liberalation Alexandra Schwatzbrod anasema ulikuwa uamuzi
mwepesi kwa gazeti lake kuchapisha picha ya kibonzo hicho.
Chanzo-BBC Swahili