Kijana
mmoja mwenye mienendo ya kustaajabisha nchini Uingereza, alipiga simu
kwa polisi baada ya kumchinja mwenzake mwenye umri wa miaka 14 ambaye
walifahamiana tu kupitia mtandao ya kijamii.
Kijana huyo alipigia polisi simu
na kuwaambia kwamba angependa waende nyumbani kwake huku wakiandamana
na wataalamu wa uchunguzi wa mauaji kwani alikuwa amemuua rafiki yake.
Kijana
huyo kwa jina Lewis Daynes mwenye umri wa miaka 19 , ametajwa na polisi
kuwa kijana hatari, mhalifu ambaye anawahadaa wenzake na kisha
kuwadhuru.
Inaarifiwa ilikuwa mara ya kwanza kwa wawili hawa
kukutana uso kwa uso kwani suiku zote mawasiliano yao yalikuwa kupitia
internet.
Daynes, alifungwa jela maisha baada ya kupatikana na hatia ya kumuua Breck Bednar mwaka jana.
Daynes
kutoka Grays, Essex, alimwalika Bednar nyumbani kwake baada ya kujuana
tu kupitia internet akimwambia alitaka sana kumuona.
Bedner alipowasili
nyumbani kwa Daynes, Daynes alimfunga mikono yake na kisha kumuua.
Taarifa hii ya kijana huyo
kuwapigia polisi simu na kuwaarifu kuhusu mauaji aliyoyafanya, imeibuka jana siku moja baada ya hukumu kutolewa dhidi yake.
'ninahitaji
polisi kuja nyumbani kwangu,'' alisema kijana huyo na alipoulizwa ikiwa
alikuwa anakiri kufanya mauaji akaseme, '' Ndio , ninakiri. ''
Baadaye
aliwapa polisi taarifa zake, jina lake na alikoishi na kisha
kuwashukuru. Alidai kwamba alimuua rafiki yake Breck baada ya kumtisha
kwa kisu.
''Sikumbuki kilichotokea lakini nilimchinja, '' aliwaambia polisi.
Baadaye polisi walifika nyumbani kwake na kumpata Daynes akiwa mtulivu huku mwili wa rafiki yake ukiwa sakafuni.
Daynes, ametajwa kama kijana
ambaye hakueleweka kitabia ila alipenda sana kutumia muda wake kwenye
kompyuta.
Wazazi wake waliachana hali iliyosababisha maafisa
wanaoshughulika maslahi ya watoto kumpeleka kwa familia ambayo sio yake
ili aweze kutuzwa.
Alikatakata nguo alizokuwa amezivaa akijaribu
kuharibu komputa aliyokuwa anaitumia ili kufuta ushahidi wa mazungumzo
waliyokuwa nayo na rafiki yake kabla ya kumuua.
Kabla ya kuwapigia
polisi simu, alimtumia mtu mmoja picha ya mwili wa Bednar ushahidi wake
kwamba amemuua.
Hata hivyo polisi wangali wanachungaza kumtambua mtu
huyo.
Mamake kijana aliyeuawa amesema anatuami kuwa kisa cha
mwanake kitakuwa funzo kwa vijana wanaojihusisha na michezo ya kwenye
internet.
Via>>BBC
Via>>BBC