HURUMA YA DEREVA KUKWEPA BATA BARABARANI,YASABABISHA AJALI MBAYA

6573294933_2188ba697b_zHuenda huruma yake kwa viumbe hawa ndiyo iliyomponza na kusababisha mauti ya watu waliokuwa katika gari alilokuwa akiendesha.


Mwanamke mmoja Emma Czornobaj raia wa Canada, amejikuta na hatia kutokana na kufanya uzembe ambao umesababisha ajali mbaya ya gari, alisimamisha gari ghafla katika barabara kuu kwa lengo la kuwaacha bata wakiwa kwenye kundi kubwa wavuke barabara na kusababisa kutokea kwa ajali na vifo vya watu wawili.

Gari lililokuwa linakuja nyuma liligonga kwa nyuma ya gari la mwanamke huyo na kusababisha kifo cha Andre Roy na binti yake Jessie mwenye umri wa miaka 16, Czornobaj alisikitika pale aliposimama na kukusanya bata wote na kuwaweka kwenye gari lake.

Mwanamke huyo alikutwa na makosa mawili, kuendesha gari kwa kasi na uzembe, amehukumiwa kukaa jela siku 90 pamoja na kuihudumia jamii kwa saa 240, pia amepigwa marufuku kuendesha gari kwa muda mwa miaka kumi.
Czornobaj
Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara moja zikitoka "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post