Hatimaye mkazi wa kijiji cha Nhelegani manispaa ya
Shinyanga Lugenzi Maguta (45), aliyeshambuliwa kwa kipigo na askari magereza wa
gereza la wilaya ya Shinyanga baada ya kuwanyima soda na biskuti amefikishwa
mahakamani na kusomewa shitaka la kufanya fujo gerezani.
Maguta amefikishwa katika mahakama ya mwanzo Shinyanga mjini
ambapo upande wa mashitaka ulimsomea shitaka la kuingia gerezani na kufanya
fujo akidaiwa kulazimisha kumpatia soda na biskuti ndugu yake aliyekuwa
mahabusu shitaka ambalo mshitakiwa amelikana.