JAMAA APANDISHWA KIZIMBANI BAADA YA KUGONGA UKUTA WA KITUO CHA POLISI

car-police_photo
Kukamatwa kwa jamaa aliyegonga ukuta wa Kituo cha Polisi akiwa anaendesha gari huenda ilikuwa moja ya kazi ambazo zilikuwa rahisi zaidi kwa Polisi wa kituo cha Frodsham, Uingereza.


Polisi wamesema jamaa huyo alikuwa amelewa, alipata ajali hiyo alipokuwa akitoka na gari yake katika eneo la Parking ambayo iko  jirani na kituo hicho, akapoteza mwelekeo na kugonga ukuta wa kituo hicho.

Polisi walimkamata na kugundua amelewa, akapandishwa kizimbani kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa.

Hakuna aliyeumia wala kujeruhiwa, ila gari na sehemu ya ukuta wa kituo hicho havikuwa na hali nzuri.

Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara moja zikitoka "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post