Chama
cha Mapinduzi CCM,kimesema hakitasita kuwachukilia hatua kali za
kimaadili wanachama na viongozi wa chama hicho ambao wameendelea na
kampeni za kuwania nafasi za juu za chama hicho ikiwemo ile ya uraisi
kabla ya wakati,kuwatahadharisha juu ya usambazi wa taarifa zisizosahihi
kwa hofu ya kuchukuliwa hatua na kuwataka kujidhibiti na kudhibiti
wapambe wao.
Akiongea na vyombo ya habari mjini Zanzibar,katibu wa itikadi uenezi
wa CCM ndugu Nape Nnauye amesema chama
hakitasita kuchukua hatua kali kwa wanachama na viingozi ambao
wameendelea kukaidi agizo la kamati kuu la kuwataka kutojihusha na
kampeni kabla ya wakati.
Aidha Nape amesema chama kimewataka wanachama na viongozi
hao,kuwadhibiti wapambe wao ambao wamekuwa wakitoa taarifa potofu pindi
vikao vya kamati kuu inapoketi na kusema kuwa chama hicho kina kazi
nyingi za kufanya si kujadili wagombea pekee.
Kuhusu kamati ya maadili iliyoketi tarehe 19 mwezi wa
kwanza 2015,Nape amesema kuwa mambo yote yaliyojadiliwa katika kamati
hiyo yatawakilishwa kwenye kamati kuu kwa kujadiliwa na ndipo yatatolewa
kwa wanannchi na kuwataka wagombea kutokuwa na hofu kama wanahisi wako
sahihi kimaadili.
Via>>Itv
Via>>Itv
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba +255 688 405 951