Kufungwa jela kwa mhalifu mwenye
tatoo kwenye jicho lake mjini Alaska kumezua gumzo sana nchini Marekani
kuhusu hatua wanazochukua waru kurembesha nyuso zao.
Bila shaka hili pia limezua gumzo kwani ni kasumba ambayo ndio imeanza kuchipuka na kuwavutia watu wengi sana.
Jason
Barnum, mwenye umri wa miaka 39, ambaye alikiri kosa la kujaribu kumuua
afisa wa polisi, ana tattoo ndani ya jicho lake kwenye paji la uso,
katika sehemu ya uso wake, kwenye meno yake na katika shavu lake.
Lakini cha kuvutia zaidi ni kuwa sehemu nyeupe ya jicho lake imewekwa tatoo kwa kutumia wino mweusi.
Upande
wa mashitaka ulisema kwamba mtuhumiwa kwa kuangalia tu uso wake uliojaa
tatoo, ni ishara kwamba ni uamuzi alioufanya kitambo sana,uamuzi wa
kuwa mhalifu.
Lakini je kwa kuweka tatoo ndani ya macho yake, alitaka kuonyesha kwamba ni mhalifu na mpenda vurugu?
Mwanamume
wa kwanza aliyejaribu kujidunga wino kwenye macho yake alikuwa mtaalamu
na mchoraji wa Tatoo, anayejulikana kama Luna Cobra.
Hakuwa na nia ya kufanana na mtu muovu bali lengo lake lilikuwa kufanana na viumbe vilivyokuwa kwenye filamu maarufu ya Dune.
''Wakati
unapodungwa ile sindano inayoweka wino kwenye macho yako unahisi kama
mtu anakudunga kisha unahisi kama mtu umewekewa mchanga ndani ya
macho,'' anasema Cobra ambaye kazi yake sasa ni kurembesha watu macho na
kuwabadilisha rangi za wacho yao. Anaishi nchini Canada.
Sindano
moja huwa na wino wa kutosha kufunika robo ya jicho. Unahitaji zaidi ya
sindano moja ya wino kubadilisha rangi ya sehemu nyupe ya jicho. Rangi
hio huwa ni ya kudumu haiwezi kutoka tena.
Kylie Garth
Kylie ana macho ya buluu na anasema kwamba watu wengi humtizama sana kitu anachokifurahia.
Kylie
anafurahishwa sana kuwa na mwonekanao wa kipekee ikizingatiwa kwamba
yeye hufanya kazi katika duka ambalo hutoa huduma kwa wanaotaka kutogwa
mjini Sydney Australia.
Kabla ya kuamua rangi ya wino aliotaka
kutumia ndani ya macho yake, Garth aliwahi kujaribu kuweka tatoo mbali
mbali ikiwemo kwenye uso wake, kutoga masikio yake na hata ulimi wake.
Jason
Barnum anasema unapobadilishwa rangi ya mambo, unahisi kama mtu
anakudunga kisha unahisi shinikizo flani halafu unahisi kama umemwagiwa
mchanga kwenye jicho lakini hauhisi uchungu wowote. ''
Hata hivyo mwanamuziki mmoja wa Poland anatofautiana na wanavyosema
wengine. Alinaswa kwenye kanda ya video akiwekwa tatoo ndani ya jicho
lake. Siku chache baadaye, alihisi kama vile jicho lake linachomeka hali
iliyomzuia hata kulala.
Garth anasema kwamba macho yake yamewapendezea wengi sana.
Labda
ni lile wazo tu la mtu kudungwa sindano ndani ya jicho lake ndilo
linawahofisha wengi. Watu huniambia, ''eeh, siamini ulifanywa hivyo.
Lakini sijawahi kusikia mtu akisema kwamba ninatisha.''
Luna Cobra
hata hivyo anasema yeye huwashauri vijana kusubiri hadi wapate kazi
kabla ya kuanza kujibadilisha rangi ya macho, kwa sababu huenda
ikawakosesha kazi. Kile alichoanza kukifanya kama jaribio la
kujifurahisha tu kwa kutaka kuwa na mwonekano wake wa kikepekee
kimewavutia watu wengi sana.
Lakini madaktari wa macho walanaani kasumba hii wakisema ni hatari na inaweza hata kumfanya mtu kupofuka.
via>>BBC
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba +255 688 405 951