MCHEKESHAJI NYOTAMBOFU MAARUFU MMASAI, ATOBOA KILICHOMKIMBIZA VITUKO SHOW

MWIGIZAJI na Mchekeshaji Bongo, Griady Kahena ‘Masai Nyotambofu’ amefunguka sababu zilizomfanya apumzike kuigiza katika Kundi la Vituko Show kuwa ni bosi wake kutowajali wasanii hasa wakiwa na shida.
“Ukiangalia Vituko Show sisi magwiji tulioanza na kundi hilo, wengi tumekimbia baada ya kuona bosi haoni umuhimu wetu pamoja na kufanya kazi lakini unaambulia maarufu tu huna pesa, una shida unaazima hata simu,” anasema Nyotambofu.
Nyotambofu ambaye kwa sasa ni mtangazaji katika kipindi cha MinBazz kirukacho katika televisheni ya Star Tv,amebainisha kuwa kufuatia utaratibu wa bosi wao kuwachukulia kama wasanii wa kawaida, wengi wamejitoa na kuangalia kazi nyingine badala ya kuigiza ili kuweza kuendesha maisha yako

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post