“Ukiangalia Vituko Show sisi magwiji tulioanza na kundi hilo, wengi tumekimbia baada ya kuona bosi haoni umuhimu wetu pamoja na kufanya kazi lakini unaambulia maarufu tu huna pesa, una shida unaazima hata simu,” anasema Nyotambofu.
Nyotambofu ambaye kwa sasa ni mtangazaji katika kipindi cha MinBazz kirukacho katika televisheni ya Star Tv,amebainisha kuwa kufuatia utaratibu wa bosi wao kuwachukulia kama wasanii wa kawaida, wengi wamejitoa na kuangalia kazi nyingine badala ya kuigiza ili kuweza kuendesha maisha yako