Wananchi
wa kijiji cha Ijoka, Mkoani Mbeya wameingia kwenye imani za kishirikina
baada ya kuandamana na kwenda kupasua mti ulianguka ambao wanadai una
utajiri ndani yake.
Wakazi hao walisema walielezwa na mganga wa jadi kutoka Malawi Peter Lungola, kuwa mti huo ukitumiwa vyema utaleta utajiri.
Mganga huyo alifika kijiji humo miaka 20 iliyopitana kuwaeleza kuw amti huo una asili kubwa ya utajiri na kuwa chini ya mti huo kuna nyumba za kifahari zilizojaa hazina kubwa ya fedha.
Inasemekana mti huo ulianguka wiki iliyopita na kuanza kupumua huku watu wakipata kiwewe huku nyoka mkubwa ambaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha.
Wazee wa kijiji hicho walishangazwa na hatua ya baadhi ya watu kula majani ya mti huo huku wengine wakichukua magome yake na kuyahifadhi majumbani mwao.
Chanzo-Kibonajoro.com
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba +255 688 405 951