MTOTO WA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA KENYA AKUTWA AMEFARIKI DUNIA KITANDANI

PrezzoFidel Odinga katikati akiwa na marafiki zake
Prezzo akiwa na Fidel Odinga katikati na marafiki wengine

Simanzi kubwa imeikumba familia ya waziri mkuu wa zamani wa Kenya Raila Amolo Odinga baada ya kutoka kwa taarifa ya kifo cha mtoto mkubwa wa mwanasiasa huyo mashuhuri nchini Kenya asubuhi ya leo .

Mtoto huyo anayefahamika kwa jina la Fidel Odinga alikutwa akiwa amefariki dunia kitandani kwake asubuhi ya leo (jumapili) baada ya kurudi nyumbani kwake alfajiri akiwa anatoka kukutana na rafiki zake .

Mara ya mwisho Fidel aliripotiwa kukutana na baba yake usiku wa jumamosi kabla ya kuagana na kwenda kukutana na rafiki zake katika sehemu ambayo haijawekwa wazi na baada ya hapo alirudi nyumbani kupumzika hadi mauti yalipomkumba .

Mwili wa Fidel Odinga ulikutwa kitandani kwake baada ya kurudi nyumbani alfajiri akiwa anatoka kukutana na rafiki zake .
Fidel Odinga

Mwili wa Fidel Odinga ulikutwa kitandani kwake baada ya kurudi nyumbani alfajiri akiwa anatoka kukutana na rafiki zake .

Hadi mauti yanamkumba Fidel Odinga alikuwa na umri wa miaka 42 na Polisi nchini Kenya wameanza uchunguzi wa kifo cha mtoto huyo wa mwanasiasa maarufu nchini Kenya huku bado kukiwa hakuna taarifa zozote kuhusiana na chanzo cha kifo chake .
Aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga.

Fidel ameacha mke mmoja na mtoto mmoja mwenye umri wa miaka miwili ambaye alizaa na mke wake Getachew Bekele ambaye ni raia wa Eritrea .

Fidel Odinga siku alipofunga ndoa na mkewe Getachew Bekele.
Fidel Odinga siku alipofunga ndoa na mkewe Getachew Bekele.

 Saa chache baada ya habari za kifo cha Fidel makundi tofauti ya watu yalianza kufanya maandamano na vurugu maeneo ya Ngong nje kidogo ya Jiji la Nairobi wakipiga kelele za ‘Nani amemuua Fidel’ wakimaanisha kuwa kifo chake kimesababishwa na mtu huku wakishindwa kutaja sababu au chanzo kamili .
Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara moja zikitoka "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post