Makubwa!!! MBWA ALIYETELEKEZWA NA BEGI KWENYE STESHENI YA TRENI APEWA OFA KIBAO

Mbwa Kai apata ofa kedekede za makazi

Mbwa aliyetelekezwa nchini Scotland ajulikanaye kwa jina la Kai amepatiwa ofa tele za makazi mapya.

Mambo yanaonekana si mabaya kwa mbwa aliyetelekezwa kwenye stesheni ya Treni akiwa na sanduku lenye mahitaji yake.

Mbwa huyu alikutwa katika Stesheni akiwa amefungiwa kwenye reli siku ya ijumaa juma lililopita.

Lakini wasamaria waliomnasua katika eneo hilo wanasema wamekuwa wakipigiwa simu mara nyingi na watu wakitaka kumpa makazi mbwa huyo.

Wasamaria wema hao wanasema Kai yuko katika hali nzuri na ni rafiki hivyo wanaamini kuwa wamiliki wa mbwa huyo ambao bado wanatafutwa walishindwa kumhudumia.

Taasisi hiyo ya msaada wa wanyama inatoa wito kuwasiliana nao kupitia namba ya msaada 03000 999 999 ikiwa kuna mtu atakuwa na taarifa kuhusu wamiliki wa Kai.

Via>>bbc 


Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara moja zikitoka  
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post