Mwanamme aitwaye jina Paul Luhende(38) ameuawa kwa kupigwa mawe fimbo sehemu mbalimbali za mwili
wake na wananchi waliojichukulia sheria mkononi baada ya kumtuhumu kuiba ng’ombe
watatu katika kijiji na kata ya Mwakitolyo wilaya ya Shinyanga vijijini mkoani
Shinyanga.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na
kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha tukio hilo limetokea
Januari 6,mwaka huu saa nane mchana.
Alisema wananchi hao waliojichukulia sheria mkononi
walimuua mtu huyo kwa kumpiga mawe na fimbo baada ya kumtuhumu kuiba ng’ombe
watatu wenye thamani ya shilingi 1,200,000/=,mali ya Subi Khamis(48) mkazi wa
Mwakitolyo.
Kamanda Kamugisha alisema chanzo cha tukio hilo ni
wananchi kujichukulia sheria mkononi na kwamba juhudi za jeshi la polisi
kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo zinaendelea.
Na Kadama Malunde-Shinyanga