Habari kutoka kitongoji cha Shatimba, kijiji cha Bugogo kata ya Mwamala tarafa ya Samuye wilaya ya Shinyanga vijijini ni kwamba watu watatu wamekutwa wameuawa na miili yao ikiwa imeharibika vibaya huku ikidaiwa huwa huenda watu hao waliuawa zaidi ya siku 5 zilizopita kwa kushambuliwa na watu wasiofahamika kisha kufungiwa ndani ya nyumba.
Malunde1 blog imeambiwa kuwa watu hao,akiwemo mwanamme
mmoja,binti na kikongwe anayedaiwa kuwa mganga wa kienyeji wamekutwa
wamekufa ndani ya nyumba na wameonekana kuwa na majeraha katika miili yao huku kichwa cha bibi kikionekana kama
kimepigwa kwa kitu kizito.
Habari zinasema kuwa miili ya watu hao imekutwa imeharibika
vibaya kwa kukatwa na vitu vyenye ncha kali vinavyodhaniwa kuwa mapanga.
Akizungumza na malunde1 blog diwani wa kata ya Mwamala Hamis Mwenda Masanja amesema miili ya watu hao imegundulika jana saa 11 jioni ambapo watu watatu wakiwemo wageni wawili binti aitwaye Christina Samweli(18) mkazi wa kitongoji cha Matanda kijiji cha Singita kata ya Usanda na mwanamme mkazi wa Karitu Nzega(hatujapata jina lake) anakadiriwa kuwa na miaka 35-40 na mwenyeji wao bibi Shija Bundala(80) walikutwa wameuawa ndani ya nyumba.
"Inavyoonekana kulikuwa na vurugu humo ndani iliyosababishwa na wauaji,na huyo mwanamme alikuwa amelala kwenye chumba kingine na wanawake chumba kingine,na pengine mwanamme alipoona kuna vurugu akatoka chumbani na mwili wa mwanamme huyo ulikutwa sebuleni huku miili ya binti na bibi ikiwa kwenye chumba walichokuwa wamelala,diwani huyo aliiambia malunde1 blog.
Taarifa kutoka eneo la tukio hilo zinasema chanzo cha tukio hilo huenda ikawa ni imani za kishirikina.
Miili ya watu hao imezikwa leo Jumapili saa tano asubuhi baada ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kuruhusu wazikwe.
"Inavyoonekana kulikuwa na vurugu humo ndani iliyosababishwa na wauaji,na huyo mwanamme alikuwa amelala kwenye chumba kingine na wanawake chumba kingine,na pengine mwanamme alipoona kuna vurugu akatoka chumbani na mwili wa mwanamme huyo ulikutwa sebuleni huku miili ya binti na bibi ikiwa kwenye chumba walichokuwa wamelala,diwani huyo aliiambia malunde1 blog.
Taarifa kutoka eneo la tukio hilo zinasema chanzo cha tukio hilo huenda ikawa ni imani za kishirikina.
Miili ya watu hao imezikwa leo Jumapili saa tano asubuhi baada ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kuruhusu wazikwe.