BIBI HARUSI AFANYA MAAMUZI MAGUMU HARUSINI,STORI INASIKITISHA!!

indian-wedding-bridal-lengha-detailed-traditional 
Bi harusi mmoja kaskazini mwa India, amejikuta kwenye wakati mgumu siku ya ndoa, kisa ni  ugonjwa wa mume wake mtarajiwa ambao yeye hakujua kama bwana huyo anaumwa.

Haikuwa siku nzuri kwa bwana harusi, ana tatizo la ugonjwa wa kifafa na tatizo hilo likamkuta siku ya ndoa yake na bibie Indra.
Indra alifanya maamuzi hayo magumu ambapo muda mfupi kabla ya kufunga ndoa na bwana Jugal Kishore, bwana huyo alianguka ghafla kutokana na kifafa na kupelekwa Hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu, tukio hilo lilimfanya Bi harusi ashikwe na hasira kutokana na mume wake huyo mtarajiwa kumficha kwamba ana tatizo la ugonjwa huo.
Indra alibadili maamuzi, akatoa ombi la kuolewa na mmoja wa wanafamilia ya bwana harusi, ambaye alikuja tu harusini kusherehekea sherehe hiyo, jamaa akaona hii ni bahati ya mtende kwake, baada ya bwana harusi kupata nafuu alirudi na kukuta story imekuwa nyingine harusini.
Hii mfano inakutokea wewe ungeamua nini mtu wangu?

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post