BINTI ANAYEDAIWA KUWA MCHAWI ANASA KWENYE NYUMBA YA MTU AKIWANGA SHINYANGA MJINI


Siku chache tu baada ya bibi aliyedhaniwa kuwa mchawi mwenye umri wa miaka 80 kukutwa nje ya nyumba ya mtu akiwa uchi huku Ndembeza mjini Shinyanga  leo binti anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23- 25 anayedaiwa kuwa ni mchawi amekutwa kwenye mlango wa nyumba ya mkazi wa mtaa wa Bushushu kata ya Lubaga katika manispaa ya Shinyanga akiwa amejifunga nguo nyeusi huku mwili wake ukiwa umepakwa dawa nyeusi usoni,mikononi,mgongoni na miguuni,alidai alikuwa anaongoza wenzake zaidi ya 10 kutoka Geita,Mwanza na Shinyanga waliofika kuwanga katika nyumba hiyo.

Binti huyo amekutwa leo asubuhi nyumbani kwa Robinson Massawe ambapo binti huyo alikutwa amelala mbele ya mlango wa nyumba hiyo akiwa hajitambui na baada ya kusemeshwa ndipo akasimulia yaliyomkuta kwamba alifika mahali hapo na wenzake kufanya sherehe baada ya kufanikisha uchawi wao wa kuharibu ndoa ya Massawe aliyegoma kuoa ndugu yao na badala yake akaoa mwanamke mwingine.

Askari wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakimhoji binti huyo

ambapo baada ya kumhoji binti huyo alisema alifika kwenye familia hiyo majira ya saa 9 usiku,akiwa kama  kiongozi wa kundi la wachawi zaidi ya 10 kutoka Ushirombo,Misungwi na Shinyanga kwa ajili ya kufanya sherehe baada ya kufanikiwa kusambaratisha kichawi ndoa ya Massawe na Mary Joseph iliyovunjika mwezi Septemba mwaka jana.
 Picha na Kadama Malunde-Shinyanga.

BONYEZA MANENO HAYA KUONA PICHA ZAIDI ZA BINTI HUYO  
AU
ALICHOKISEMA BAADA YA KUKAMATWA 






Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post