Raia mmoja wa Uturuki aliganda na
kuwa barafu baada ya kujaribu kuingia ndani ya ndege ili kwenda kumuona
mpenziwe nchini Uingereza.
Hikmet Komur mwenye umri wa miaka 32
alitamani sana kumuona mpenziwe Luisa da Silva suala lililomlazimu
kupanda katika gea ya kutua kwa ndege moja ya Uingereza nchini Istanbul.
Lakini alifariki alipokuwa katika safari kutokana na baridi kali ya vipimo vya chini vya -60c ambayo ilimuathiri ubongo wake.
Kabla ya safiri alimwambia mwanae kwamba atasafiri kwa siku chache.
Mwili
wa bwana Komurs ulipatikana katika uwanja wa ndege wa Heathrow baada ya
wafanyakazi katika uwanja huo kuona miguu ya binadamu.