|
Jumla
ya risasi 356 za SMG/SAR zilizokamatwa askari Polisi kwa kijana mmoja
aliyefahamika kwa jina la Wolfram Msemwa(32) huko katika mtaa wa
Kazehill kata ya Ng'ambo manispaa ya Tabora.
|
|
|
Risasi hizo
|
|
Kitambulisho
cha mtuhumiwa aliyekutwa na risasi hizo ambaye kabla ya kukamatwa
tarehe 2/2/2015 aliwahi kuwakimbia askari Polisi mnamo tarehe
23/11/2014 na kutelekeza begi alilokuwa amehifadhi bunduki aina ya SMG
na risasi 17 katika eneo la Mazinge hospitali ya wilaya ya Sikonge |
|
Kaimu
kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Juma Bwire akiwaonesha waandishi
wa habari risasi zilizokamatwa katika operesheni maalumu iliyofanikiwa
kumtia nguvuni kijana huyo Wolfram Msemwa anayedaiwa amekuwa na mtandao
na baadhi ya waharifu kutoka nchi jirani na Tanzania kwa upande wa
Magharibi. |
Jeshi
la polisi mkoani Tabora limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa wa matukio ya
uharifu huko katika kata ya ngambo manispaa ya Tabora, akiwa na risasi
356 za silaha za SMG/SAR, zilizosadikiwa kuwa, zilikuwa zitumike, katika
matukio ya uharifu katika mikoa ya Tabora, Kigoma ,Mbeya, na Njombe.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani Tabora kamishima msaidizi Juma Bwire
amemtaja mtuhumiwa huyo kwa jina la Warfram Benard Msemwa, mkazi wa Sikonge, ambaye alikuwa akitafutwa na jeshi hilo kutokana na kutelekeza
begi lililokuwa na silaha aina ya SMG na risasi 17, huko katika eneo la
kituo cha afya cha Mazinge wilayani humo.
Aidha Acp Juma Bwire amesema kuwa, katika kumhoji mtuhumiwa huyo
amekiri kuwa na mawasiliano ya kiuharifu na watu furani katika nchi
jirani ya Burundi ambapo zinatoka risasi hizo pamoja na siraha, ambayo
aliiteklekeza hapo awali kwa kuwahofia polisi aliowaona kwa mbali, na
upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553