Hatari!! MWANAMKE AMUUA KWA KUMCHOMA KISU MPENZI WAKE ALIYETAKA KUMPIGA CHINI!!

KnifeInapotokea hali ya kutoelewana katika uhusiano ni mara chache sana wote wawili kukubali kwamba uhusiano huo ufike mwisho, lakini mara nyingi mmoja yao huwa hakubaliani kirahisi na uamuzi huo.

 
Mwanamke mmoja China, Azuha Kikuchi amekamatwa baada ya kumuua aliyekuwa mpenzi wake, Yuji Hirata ambaye walikuwa wanaishi jengo moja kwa kumchoma kisu kifuani.

Polisi wamefanya uchunguzi na kugundua Kikuchi alimpiga mwanaume huyo kichwani  na kumchoma na kisu kifuani ambapo mwili wake ulikutwa ndani ya chumba chake ukiwa na majeraha na walipomfikisha Hospitali alikuwa tayari amefariki.

Kikuchi alipohojiwa alikubali kuhusika na tukio hilo na kuwaambia Polisi kuwa kulitokea hali ya kutoelewana baada ya mpenzi wake kutaka kuvunja uhusiano wao.

Ndani ya chumba hicho kulikutwa pia fimbo yenye wavu wa kuchezea tennis ukiwa na damu pamoja na kisu kilichokuwa kwenye begi ambavyo vilinunuliwa na Kikuchi siku chache kabla ya tukio hilo kutokea.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post