Mauaji Tena Shinyanga Vijijini !! MWINGINE AUAWA KWA KUKATWA MAPANGA USIKU WA MANANE AKIWA AMELALA NYUMBANI KWAKE

Siku tatu tu baada ya watu watatu kuuawa kwa kukatwa mapanga kisha kufungiwa ndani ya nyumba zaidi ya siku 5 katika kijiji cha Bugogo wilaya ya Shinyanga,mauaji ya watu wa kukatwa mapanga yameendelea kujitokeza ambapo huko katika kijiji cha Manyada,kata ya Usanda wilaya ya Shinyanga mwanamke mmoja ameuawa kwa kukatwa mapanga akiwa amelala nyumbani kwake.

Tukio hilo limetokea jana saa nane usiku.

Kamanda  wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Justus Kamugisha(pichani) amemtaja aliyeuawa kuwa ni Winifrida Simon(35) ambaye alivamiwa akiwa amelala ndani ya nyumba yake na watu wasiofahamika kisha kukatwa mapanga kichwani na shingoni.


Amesema chanzo cha mauaji hayo bado kinachunguzwa na kwamba tayari watu wanne wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi  kuhusiana na tukio hilo.

Kamanda Kamugisha amewataja wanaoshikiliwa na polisi kuwa ni Misana Juma(30),Joseph Jahila(24) Emmanuel Joseph(39) na Msafiri Kulwa wote wakazi wa Manyada kata ya Usanda tarafa ya Samuye wilaya ya Shinyanga.

Na Kadama Malunde-Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post